Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Anthony Mtaka, Akizungumza pamoja na wakazi wa eneo la Kingolwira pamoja na wageni mbalimbali waliotoka sehemu mbalimbali Tanzania na kutoa tamko rasmi la kuzindua shindano la Maisha Plus/ Mama shujaa wa chakula 2013
Friday, 3 January 2014
DC MVOMERO AFUNGUA MKUTANO WA WASABATO TURIANI MOROGORO.
DC Mtaka akizngumza na Mkurugenzi wa Global Mission kutoka Ukraine Mchungaji Dmitry Zubbkov kulia na katikati ni Dkt Alex Magufwa baada ya mkuu huyo kumaliza kufungua mkutano Mkuu wa dini unaofanyika katika vijiji viwili vya Kialawa na Lukenge na ambapo wananchi wa maeneo ya jirani mkoani hapa, kulia ni mchungaji wa mtaa wa kanisa hilo, Leonard Mbushi na katikati ni mkuu wa wilaya mstaafu wa Kwimba mkoani Mwanza, Reuben Matongo.
Sehemu ya watoto katika kijiji cha Kialawa na waumini wa kanisa hilo wakifuatia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi huo.
Kwaya ya kanisa hilo la Kialawa wakitumbuiza kwa nyimbo za mapambio.
Mkurugenzi wa Global Mission kutoka Ukraine Mchungaji Dmitry Zubbkov kulia akifafanuliwa jambo kutoka kiswahili na KiUkraine na Dkt Alex Magufwaambaye ni mwenyeji wake wakati mkuu wa wilaya ya Mvomero akifungua mkutano huo wa dini.

MKUU WA WILAYA YA MVOMERO MHE ANTHONY MTAKA AKIAPA MBELA YA MKUU WA MKOA WA MOROGORO MHE JOEL BENDERA

MHE ANTHONY MTAKA AKIKABIDHIWA ZAWADI YA MAUA NA MAMA YAKE MZAZI KATIKA HAFLA HIYO
Monday, 30 December 2013
RAIS KIKWETE KATIKA HAFLA YA KUKABIDHIWA RASIMU YA KATIBA LEO
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali wakiwapongeza wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya katiba baada ya makabidhiano ya Rasimu ya pili ya Katika katika viwanja vya Karimjee Hall jijini Dar es salaam
Picha ya pamoja na wajumbe wa tume
Rais Kikwete akizungumza na Mwenyekiti wa CUF Prof Ibrahim Lipumba na wa NCCR Mageuzi Mhe James Mbatia mara baada ya kukabidhiwa na Rasimu ya katiba mapema leo,ambapo hafla hiyo imefanyika viwanja vya Karimjee jijini Dar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Kitaifa,Wanasiasa na Wanaharakati,Shoto ni Waziri mkuu Mstaafu,ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba akishuhudia.PICHA NA IKULU
Subscribe to:
Posts (Atom)